Zaburi 134
Wito Wa Kumsifu Mungu
Wimbo wa kwenda juu.
Msifuni Bwana, ninyi nyote watumishi wa Bwana,
ninyi mnaotumika usiku ndani ya nyumba ya Bwana.
Inueni mikono yenu katika pale patakatifu
na kumsifu Bwana.
 
Naye Bwana, Muumba wa mbingu na dunia,
awabariki kutoka Sayuni.