113
Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe. Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele. Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe. Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni. Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu, atazamaye chini angani na duniani? Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani, ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake. Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!