112
Msifuni Yahwe. Amebarikiwa mtu yule anaye mtii Yahwe, apendezwaye sana na amri zake. Kizazi chake kitakuwa ni chenye nguvu duniani; kizazi cha mcha Mungu kitabarikiwa. Nyumbani mwake mna utajiri na mali; na haki yake itadumu milele. Nuru huangazia gizani kwa ajili ya mtu mcha Mungu; yeye ni wa fadhili, huruma, na haki. Heri atendaye fadhili na kukopesha, afanyaye mambo yake kwa uaminifu. Kwa maana hataondoshwa kamwe; mwenye haki atakumbukwa milele. Haogopi habari mbaya; ni jasiri, akimtumainia Yahwe. Moyo wake ni mtulivu, hana woga, mpaka aonapo ushindi dhidi ya watesi wake. Huwapa masikini kwa ukarimu; haki yake yadumu milele; atainuliwa kwa heshima. 10 Mtu mwovu ataona haya na kukasirika; atasaga meno yake na kuyeyuka; tamaa ya wasio haki itapotea.